MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'AFIRITI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA NENO 'AFIRITI
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AFIRITI'

Neno *afiriti*[ *Ngeli: a-/wa-]* katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana zifuatazo: ya:

1. Mtu anayechochea wenzake kufanya maovu.

2. Shetani aletaye madhara kwa watu, maluuni, jini, ibilisi.

3. Mtu mwenye tabia za ujanjaujanja, mdangayifu.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *afiriti* (soma: *ifriit عفريت)* ni nomino yenye maana zifuatazo:

1. Mtu khabithi/habithi, muovu, mdaganyifu.

2. Mtu mwenye ujuzi wa hali ya juu katika kutenda jambo fulani; mahiri.

3. Jini, shetani, pepo.

4. Kreni inayoinua magari na kadhalika.

Kinachodhihiri ni kuwa neno *afiriti* ( *soma: ifriit  عفريت*) lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *afiriti* maana zake zinazohusu jini na mtu mjanjamjanja/mdanganyifu hazikubadilika isipokuwa limeacha maana zingine katika Kiarabu na kuchukua dhana ya mtu anayechochea wenzake kufanya maovu.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)