12-31-2021, 09:52 AM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AFIRITI'
Neno *afiriti*[ *Ngeli: a-/wa-]* katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana zifuatazo: ya:
1. Mtu anayechochea wenzake kufanya maovu.
2. Shetani aletaye madhara kwa watu, maluuni, jini, ibilisi.
3. Mtu mwenye tabia za ujanjaujanja, mdangayifu.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *afiriti* (soma: *ifriit عفريت)* ni nomino yenye maana zifuatazo:
1. Mtu khabithi/habithi, muovu, mdaganyifu.
2. Mtu mwenye ujuzi wa hali ya juu katika kutenda jambo fulani; mahiri.
3. Jini, shetani, pepo.
4. Kreni inayoinua magari na kadhalika.
Kinachodhihiri ni kuwa neno *afiriti* ( *soma: ifriit عفريت*) lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *afiriti* maana zake zinazohusu jini na mtu mjanjamjanja/mdanganyifu hazikubadilika isipokuwa limeacha maana zingine katika Kiarabu na kuchukua dhana ya mtu anayechochea wenzake kufanya maovu.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *afiriti*[ *Ngeli: a-/wa-]* katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana zifuatazo: ya:
1. Mtu anayechochea wenzake kufanya maovu.
2. Shetani aletaye madhara kwa watu, maluuni, jini, ibilisi.
3. Mtu mwenye tabia za ujanjaujanja, mdangayifu.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *afiriti* (soma: *ifriit عفريت)* ni nomino yenye maana zifuatazo:
1. Mtu khabithi/habithi, muovu, mdaganyifu.
2. Mtu mwenye ujuzi wa hali ya juu katika kutenda jambo fulani; mahiri.
3. Jini, shetani, pepo.
4. Kreni inayoinua magari na kadhalika.
Kinachodhihiri ni kuwa neno *afiriti* ( *soma: ifriit عفريت*) lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *afiriti* maana zake zinazohusu jini na mtu mjanjamjanja/mdanganyifu hazikubadilika isipokuwa limeacha maana zingine katika Kiarabu na kuchukua dhana ya mtu anayechochea wenzake kufanya maovu.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda