MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA MANENO 'ADUI', 'ADAWA' NA 'UADUI'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA MANENO 'ADUI', 'ADAWA' NA 'UADUI'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO 'ADUI', 'ADAWA' NA 'UADUI'

Neno adui (wingi: maadui) katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:

1. Nomino: Mtu, mnyama au kiumbe chochote kinachofanyia kiumbe kingine uovu.
Kuna methali: adui wa mtu ni mtu, adui mpende, adui aangukapo mnyanyue.

2. Nomino: Mtu unayekabiliana naye katika mchezo.

3. Nomino: Jambo, kitu au hali inayokuletea madhara.
Kuna msemo: Ujinga ni adui wa maendeleo.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili adui (soma: aduwwun/aduwwan/aduwwin عدو ) ni nomino yenye maana ya "mwenye uadui, chuki au hasama dhidi mwengine."

Neno adawa katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana ya:"hali ya kufanya chuki dhidi ya mtu mwengine."

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili adawa (soma: adaawatun/adaawatan/adawaatin عداوة ) lina maana zifuatazo:

1. Nomino: Hali ya kufanyianana uadui, chuki na hasama baina ya pande mbili au zaidi.

2. Nomino : Chuki,

Ama neno ' uadui ' limetoholewa kutoka neno ' adui ' na kupewa maana zifuatazo:

1. Hali ya kufanyiana mambo mabaya baina ya watu wa pande mbili.

2. Hali ya watu kuchukiana na kutendeana maovu.

3. Ukosaji huruma, tabia ya kutenda mambo ya ukatili.

Neno hili uadui kwa maweko yake, si neno la Kiarabu.

Kinachodhihiri ni kuwa maneno adui (soma: aduwwun/aduwwan/aduwwin عدو) na adawa (soma: adaawatun/adaawatan/adaawatin عداوة) yalipoingia katika lugha ya Kiswahili na kutoholewa kuwa maneno adui na adawa maana zake za msingi katika Kiarabu hazikubadilika.

Shukran sana.

Khamis S.M. Mataka.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)