MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'MASKANI'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'MASKANI'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO ' MASKANI'.

Neno Maskani katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana zifuatazo:

1. Mahali kiumbe anapoishi kama vile nyumba au eneo.

2. Mahali ambapo watu aghalabu wafuasi wa chama fulani cha siasa hukutana na kuzungumza.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili (maskani) lina maana zifuatazo:

1. Makazi/Makaazi.

2. Nyumba.

Katika Sarufi ya Kiarabu kinapoongezwa kiambishi 'ma' mwanzoni kwa neno la msingi (mzizi) hutengeneza neno lenye maana ya eneo linapofanyika tendo linalohusiana na maana ya mzizi huo na hasa mzizi wa kitenzi.

Kwa mfano neno la Kiarabu 'darasa درس' (amesoma) kinapoongezwa kiambishi 'ma' mwanzoni kwa Sura ya neno (maf-al/maf-il) yaani (madrasa مدرسة) hutengeneza neno (nomino) lenye maana ya mahali tendo la kusoma hufanyika.

Pia kitenzi cha Kiarabu kataba كتب (ameandika), kinapoongezwa kiambishi 'ma' kwa namna iliyotangulia kuelezwa hupatika neno (maktab/maktaba مكتب/مكتبة) lenye maana ya mahali ambapo kitendo cha kuandika hufanywa. Ndipo neno hili (maktab/maktaba) katika Kiarabu likapata maana ya ofisi, dawati, meza ya kuandikia, mahali panapohifadhiwa vitabu kwa nia ya kujisomea.

Ndipo pia tunapata kutokana na kitenzi cha Kiarabu 'sakana سكن' (amekaa/amefanya makazi) baada ya kuongezwa kiambishi 'ma" mwanzoni mwake neno 'maskani مسكن' lenye maana ya mahali pa kukaa/makazi.

Utaona kuwa neno hili 'maskani' lilipoingia katika lugha ya Kiswahili limeongezewa maana ya mahali ambapo watu hukutana na kuzungumza.

Shukran sana.

Khamis S.M. Mataka.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)