MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MFANO WA SOGA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
MFANO WA SOGA
#1
KIFENGE NA BARUA KWENDA KWA BWANA MUNGU
Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Kifenge alikuwa maskini sana. Yeye na familia yake waliishi kwa kuombaomba chakula, mavazi na mahitaji mengine.
Siku moja wazo la kuomba msaada kutoka kwa Bwana Mungu lilimjia. Kifenge alienda dukani akanunua karatasi,bahasha na stempu akaamua kumwandikia Bwana Mungu barua.
Barua ilipofika posta wafanyakazi wa posta wakashangaa kuona  barua inatakiwa kutumwa kwa Bwana Mungu. Wakaifungua wakaisoma,wakamhurumia sana Bwana Kifenge. Wakaamua kuchanga fedha hadi zikafika laki tano,wakazituma katika anwani iliyokuwa kwenye barua.
Baada ya wiki moja fedha zikafika kwa Kifenge. Alifurahi sana na akamwambia mke wake, “Mke wangu sasa dhiki imeisha. Tununue mahitaji yote, tukae, tustarehe.”
Mke wake alifurahi sana akamuuliza mume wake, “Hivi siku zote tulikuwa wapi mume wangu? Kumbe ndiyo maana watu wanatajirika lakini hawasemi kama Bwana Mungu huwa anawatumia fedha?”
Wakanunua magunia ya mchele, sukari, unga, mafuta na nguo na mahitaji mengine mpaka fedha zote zikaisha.
Fedha zilipoisha na mahitaji yakaisha wakaandika barua ingine kwa Bwana Mungu kuomba msaada. Wafanyakazi wa posta walipoiona wakajua mwandishi ni yuleyule. Wakamjibu, fedha ulizopata kama hukuweka mtaji, hakuna fedha tena.
Bwana Kifenge alipoipata akazunguka kila mahali akitangaza kuwa atawashitaki wafanyakazi wa posta kwa sababu wameiba fedha zake alizotumiwa na Bwana Mungu. Hata hivyo wenye akili wakasema kweli wajinga ndio waliwao. “Hivi Kifenge hakujua kuwa ule ulikuwa ni msaada uliotoka kwa watu wema ambao alitakiwa kuutumia vizuri?”
Kelele za Kifenge hazikuzaa matunda, akarudia umaskini wake kama zamani.
Kutokana na hadithi ya Kifenge tunaona kuwa Soga ni hadithi fupi za kuchekesha au kukejeli. Mara nyingi wahusika wake ni watu wa kubuni, na huwa na kisa kimoja tu.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)