MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ASILI YA NENO "MZUNGU"

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ASILI YA NENO "MZUNGU"
#1
Kuna mtu hivi punde aliniuliza?

Nna swali kuhusu neno 'mzungu' je maana yake haswa ni nini na kiasiliĀ  laweza kuwa latoka wapi? Fursi?

Nami nikamjibu?

Waalaykum salaam. Asili yake ni Kiswahili; si Kifursi. Mzi(zi) wa neno hilo ni "zung-". Kutokana na mzi huo ndio twapata vitenzi: zungua, zunguana, zungulia, zunguliwa, zunguka, zungusha; na kadhalika. Na twapata nomino (majina): mzunguaji, mzunguliwa, mzunguka, mzungusha; au mzungu, kizungu, uzungu, na kadhalika.

Pengine utauliza: Vilikuwaje hata Mswahili akamwita huyu mtu "mweupe" kutoka Ulaya "mzungu"? Kuna nadharia tatu:

Ya kwanza ni kwamba mtu huyu alipokuja Uswahilini, au Afrika kwa jumla, hakutulia mahali pamoja, bali alizungukazunguka kutafuta mahali pamfaapo kukita hema lake au kukipata kile alichokuwa akikitafuta - khaswa utajiri wa nti zetu. Kwa hivyo, kutokana na kuzungukazunguka kwake, akaitwa mzungu; yaani mzungukaji.

Nadharia ya pili yatokana na maana ya pili ya neno "mzungu" (wingi wake ni "mizungu") - neno ambalo likitumika katika Kiswahili hata kabla ya mtu mzungu kuja pande za kwetu. Na maana hiyo ndiyo ambayo kwa Kiingereza huitwa "trick." Kwa vile mzungu alipokuja makwetu, mbali na kutumia nguvu za silaha, ndia nyengine aliyoitumia ili kutawala ilikuwa ni urongo na kuwahadaa wenyeji ili apate kuwatawala. Kwa hivyo, akaitwa "mzungu" kwa maana ya kwamba ni mtu wa kuhadaa watu - a man of tricks.

Nadharia ya tatu ya kwa nini aliitwa "mzungu" yatokana na neno la kale la Kiswahili, "mzungupule" ambalo maana yake ni mtu mwerevu; na uwerevu ni uzungupule. Kwa vile mzungu alipokuja makwetu watu walimuona kuwa ni mtu mwenye akili na ajuaye mambo mengi, basi wakamwita "mzungu"; yaani mtu mwerevu, mwenye akili. Sijui ni ipi kati ya hizo tatu ndiyo nadharia ya sawa.

Natumai nnafahamika, ingawa nnayaandika haya haraka haraka na bongo langu hivi sasa lashughulika zaidi na kujiuguza; halikutulia.

~ Abdilatif Abdalla
Hamburg, Ujarumani
6 Juni 2019
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)