MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KULIPA GHARAMA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
JIFUNZE KULIPA GHARAMA
#1
ACHA KUPENDA VYA BURE !!!!
(Pamoja na urefu wake nakusihi ujipe muda kusoma mpaka mwisho)
Makala aliyoandika Paul Mashauri siku chache kabla ya kifo cha Ally Mufuruki. (Mufuruki the legend).
Miaka 10 iliyopita nilimfuata Mr. Ally Mufuruki, Mwenyekiti, CEO, Round Table ofisini kwake. Nikamwambia Mr. Ally unajua tunavyojaribu kusaidia watanzania wenzetu wapate maarifa kupitia “East Africa Speakers Bureau”. Nakuomba sana uje uzungumze katika kongamano tunaloandaa kwa wafanyabiashara. Akaniambia Paul hakuna tatizo juu ya hilo, lakini ada yangu “speaker fee” ni Tsh. milioni 2. Sikumuelewa kabisa Mr. Mufuruki hasa ukizingatia ukweli kwamba anapenda maendeleo ya watanzania wenzake na angeweza kuongea bure.
Lakini haikunichukua muda kumuelewa Mr. Mufuruki. SIku moja mimi mwenyewe binafsi nikaandaa semina ya bure. Gharama zote nilibeba mwenyewe lakini walifika watu 5 tu. Nilistaajabu ya dunia. Semina ambayo hutoza mshiriki mmoja Tsh. 350,000/= na ukumbi unajaa wamekuja watu 5 tu angali semina hiyo hiyo ni bure. Nikagundua watu hawathamini kitu wanachopata bure. Ndiyo maana Mr. Mufuruki alikataa kuongea bure. Sio kwa sababu ya pesa, ni kwa sababu hana muda wa kupoteza. Vitu vya bure vingempotezea muda wake. Nikajifunza kitu kipya kwenye maisha yangu. Ukitaka jambo lako lithaminiwe acha watu walipe gharama.
Somo nililolipata kwa Mr. Mufuruki likawa sehemu ya maisha yangu. Miaka kadhaa ikapita nikafuatwa na binti mmoja na kaka mmoja. Walikuwa ni watu maarufu sana katika nchi hii. Wenye ushawishi mkubwa kwa vijana “celebrities”. Wote walikuwa na mawazo ya biashara na walitaka niwe “mentor” wao. Nikawaambia sawa. Lakini kabla sijaanza “mentorship” program hii, naomba kila mmoja wenu aandike hilo wazo katika “business plan” na atengeneze mfano au “demo” itokanayo na hilo wazo, kisha atafute angalau wateja 2 ndio tuanze “mentorship”. Waliondoka moja kwa moja hawakurudi tena.
Sikuwaambia wale vijana wafanye yote hayo kwa sababu nilikuwa siwezi kuwatengenezea “business plan” au kuwatafutia wateja. Saa 12 tu kwangu zingetosha kuwapa “business plan” yenye mashiko na ningepiga simu chache tu kwenye “network” yangu kuwaunganisha na wateja. Niliwaambia wafanye yale yote ili walipe gharama. Ili waone thamani ya “mentorship” program wanayoitaka. Ili watilie maanani kile wanachotaka kujifuna kutoka kwangu. Kama Mr. Mufuruki alivyotaka mimi na wale niliokuwa nawaandalia kongamano waone thamani ya muda wake na maarifa aliyonayo na mimi nilitaka hawa vijana waone thamani ya muda wangu na kile wanachohitaji ili kuishi ndoto zao.
Kupenda vitu vya bure, kupenda mteremko ni chanzo cha umasikini. Kwa sababu vitu vya bure vinakuja kirahisi. Hautumii nguvu, hautumii akili wala hautokwi jasho. Ukiangalia duniani jamii ambazo zimefanikiwa sana kiuchumi ni jamii ambazo ili uishi, ili upate chakula, ili upate mahala pa kulala ni lazima utumie nguvu zako, akili zako, maarifa yako. Hakuna vitu vya bure. Hakuna mteremko. Kwa kifupi ni lazima ulipe gharama. Ndiyo maana mataifa kama Uingereza na Marekani, huwezi kuishi kama huna kazi inayoeleweka. Wakati mwingine lazima ufanye kazi zaidi ya moja. Ndiyo maana nchi kama Japan, haina rasilimali nyingi lakini ni moja kati ya mataifa yenye uchumi wenye nguvu. Ni kwa sababu kuna changamoto nyingi sana kiasi kwamba kama huna ubunifu huwezi kuishi. Ndiyo maana watu kutoka nchi kama India na China wamesambaa dunia nzima. Ni kwa sababu huko kwao wako wengi sana kiasi kwamba ili utoke kimaisha ni lazima ufanye kitu cha tofauti.
Na kwa mtazamo huohuo ukiangalia jamii masikini sana duniani ni zile jamii ambazo watu wanapenda vitu vya bure. Wanapenda vya kupewa. Ni jamii ambazo hata kama hutaki kufanya kazi utaishi. Kwa sababu ukiumwa njaa utaenda kwa mjomba atakupa hela, utampiga mzinga shemeji yako atakupa hela, utatafuta mke kutoka familia bora utapata hela, utatafuta mume wa mtu akuweke nyumba ndogo upate hela, au utaingia barabarani kuwa ombaomba upate hela ya chakula. Ni jamii ambazo ombaomba wana akiba ya fedha “savings” kuliko wenye mishahara. Ni jamii ambazo maisha siyo magumu. Ni jamii ambazo watu wazembe wanaona ni wajibu wa wale wanaojituma na kutokwa jasho kuwapa hela za kujikimu angali wao wanakesha baa wanakunywa mbege na wanzuki. Ni maisha yasiyo na utofauti na chawa. Maisha ya kunyonyana damu.
Hakuna ubaya kwenye kusaidiana katika maisha. Wala hakuna ufahari kwenye kufanikiwa kwa kutokwa jasho. Lakini ukweli ni kwamba kula kwa jasho ni amri iliyotoka kwa Mungu mwenyewe. Kula kwa kutumia kazi za mikono mikono yako ni amri iliyotoka kwa Mungu mwenyewe. Asiyefanya kazi na asile ni amri iliyotoka kwa Mungu. Hatukatai! Unaweza ukapewa kitu cha bure lakini usifanye kuwa ni sehemu ya utamaduni wako. Kwa sababu akili yako ikifika hatua ikaona kupata vya bure ni haki yako, utachukia watu pasipo sababu za msingi na utaona ni bore ufe kuliko kuishi. Kumbe uwezo wa kupila gharama na kutoka kimaisha uko ndani yako.
Unapokataa kumpa mtu kitu cha bure haumnyanyasi unamsaidia. Hata mtoto mdogo ana umri wa kutafutiwa chakula na kulishwa. Lakini ukitaka umtafutie mtoto wako chakula na kumrisha maisha yake yote hata akishaota ndevu haumsaidii unamharibu. Hivyo ndivyo nilivyowafanyia wale vijana wawili waliokuja kwangu wanataka “mentorship”. Ningewatengenezea “business plan” na kuwatafutia “wateja” ningekuwa siwasaidii ningewaharibu. Kwa sababu “business plan” na “wateja” ni sehemu ndogo sana ya kufanya baishara. Kuna kuishi na wafanyakazi, kuna kuishi na mabenki, kuna kupambana na changamoto za kuibiwa nk. Zaidi ya hapo, mimi ni binadamu, nina matatizo yangu na ninafamilia inaniangalia. Siwezi kuwa sehemu ya maisha ya wale vijana milele hata kama nina roho nzuri kiasi gani. Lazima waonyeshe kiu na njaa ya kutaka kuishi ndoto yao kabla sijaingiza maarifa na muda wangu katika maisha yao.
Sio mimi tu na Mr. Mfuruki tulio na mtazamo huu. Nakumbuka pia siku moja nilikuwa na rafiki yangu, Partner wa KPMG. Akaniambia wanapotafuta wafanyakazi, moja kati ya vigezo ni kuona “attitude” zao. Hata kama huyu mtu ana akili kiasi gani kama “attitude” yake si nzuri wanaweza wakamuacha. Akasema wakati mwingine unaweza ukamuita mtu kwa ajili ya “interview” lakini unamuacha akae kwanza “reception” muda wa “appointment” yake upite tena sana ili uone uvumilivu wake. Sio kwamba unamtesa au unakuwa “unprofessional”. Hapana, ni sehemu ya “interview”. Kama mtu hawezi kuvumilia masaa 3 mbele ya muda aliopewa wa “interview” ataweza kuvumilia “etra hours” akiwa kazini?
Rafiki yangu wa KPMG akawa ameniongezea kitu ambacho Mr. Mfuruki alinifundisha. Kwamba ukipata kitu kwa mteremko huwezi kukithamini. Hata mtu anayepata kazi kwa mteremko hawezi kithamini ile kazi. Ingekuwa ukimaliza tu chuo unapigiwa simu njoo uanze kazi kwa mshahara wa milioni 30 inawezekana wengi wetu wasingethamini kazi zao. Lakini ule mchakato wa kutembea na bahasha ya kaki, kuomba “interview” na kukosa, kuitwa kwenye “interview”, kufanya “interview” ya kwanza na ya pili na ya tatu inakufanya uiheshimu kazi. Kwa sababu kufuatilia kazi miezi sita ni kulipa gharama. Ni sawa na kumlipa Mr. Mfuruki shilingi milioni 2 aje kuzungumza kwenye kongamano lako. Yale atakayofundisha utayatilia maanani. Kwa sababu umelipa gharama.
Mambo ya msingi kwenye maisha utakutana nayo kila mahali. Kulipa gharama ili utoke maishani ni jambo la msingi ukubali au ukatae. Hata wewe usikubali kutoa ulichonacho bure hata kama ni mawazo. Hata kama hauhitaji chochote weka gharama fulani anayehitaji ulichonacho alipe. Akikipata kwa jasho atakiheshimu. Nililiona hilo kwa Mfuruki, kwa rafiki yangu Partner wa KPMG na nikaja nikaliona tena kwa Dr. Reginald Mengi. Siku moja nikiwa ofisini kwake akaanza kulalamika. Akasema “hebu anagalia hawa vijana wa siku hizi walivyo wa ajabu. Kuna kijana hapo “reception” baba yake amemtuma kwangu nimpe kazi. Mimi nina vikao. Amekaa hapo masaa 2 ameshampigia simu baba yake kwamba mimi nimemueweka tu hapo reception masaa 2. Huyu ameshashindwa “interview”. “He is a baba’s boy”.
Kama ilivyokuwa kwa Mr. Mfuruki Dr. Reginald Mengi alitaka kuuthaminisha mchakato wa yule kijana kupata kazi. Sio kwa sababu baba wa yule kijana anafahamiana na Dr. Mengi basi kazi ipatikane kirahisi. Huo sio utamaduni wa mafanikio. Watu waliopitia michakato ya kufanikiwa kama Mr. Mfuruki na Dr. Mengi wanata
mbua hilo. Ndivyo nchi zilizoendelea zilipotokea. Wanatambua umuhimu wa kulipa gharama. Wanakimbia utamaduni wa kutaka vya bure. Wanaheshimu amri ya kula kwa jasho, kula kwa kazi za mikono yako na asiyefanya kazi na asile.
Nimeandika makala hii kwa sababu hii sio elimu ambayo utafundishwa darasani. Hata mimi sikufundishwa na Professor wangu wa uchumi. Nimefundishwa mtaani. Somo lilipoiingia vizuri na mimi nikaanza mchakato wa kufundisha wengine. Ndio maana hata mimi huwezi kunipata kirahisi. Huwezi kuandika tu msg. facebook naomba kukuona nikasema njoo kesho. Sio Mashauri huyu. Sio kwa sababu sina muda. Muda unatengenezwa na unapatikanika. Kama napata muda wa kuandika kwanini nikose muda wa kuonana na wewe? Lakini nataka nijirizishe kwamba uko tayari kulipa gharama. Nataka nijue kama kweli una njaa na hicho unachokitaka, una kiu ya kukifanikisha au unataka kunipotezea muda wangu.
Hata wale ninaofanya nao kazi au niliowahi kufanya nao kazi watakuambia. Wanalipa gharama. Ndio maana wapo vijana wengi leo hii wamesimama wao kama wao wakiwa na biashara zao lakini watakuambia nilijifunza nilipofanya kazi kwa Mashauri. Wengine ni wakuu wa wilaya na wengine ni mawaziri. Ni kwa sababu sikuwaacha wasubiri kulishwa kama watoto wadogo angali wameshaota meno. Nilihakikisha hawapati mteremko walipokuwa na mimi, nilihakikisha wanatoka jasho, wanapanda milima na mabonde. Nilikuwa nawafundisha kujitegemea. Hilo ndio somo ambalo wengi hawalitaki, lakini hilo ndio somo pekee mbalo linaweza likakuvusha kutoka hapo ulipo kuelekea kule unapotaka kufika.
kama umeweza kusoma makala hii ndefu namna hii na kuimaliza ina maana wewe hupendi mteremko na nataka nikutie moyo ya kwamba utafika mbali kwenye maisha yako. Wengi wakiona makala ndefu kama hii hawasomi. wanaandika chini kwenye-comments “gazeti”. Ni kwa sababu wanapenda mteremko. Wanapenda kusoma vile vitabu vya “How to Get Rich Quicker”. Wanapenda kusoma “tweets” yenye sentensi mbili. Bahati mbaya sana maisha siyo “twitter”, maisha hayana shortcut.
Ndio maana matangazo ya “tender” za biashara na kazi hayako “twitter” yako kwenye magazeti. Kwa sababu ili usome gazeti kama hii makala ni lazima uwe na njaa, uwe na kiu ya kufikia malengo yako. Ndio maana “page” kama zangu haziwezi kuwa na “followers” wengi kwenye “social media” ukilinganisha na “comedy”. Kwa sababu masomo yangu hayana mteremko. Lazima ufikiri ndio uelewe. Unaweza ukasoma “post” yangu usiku ukaitafakari usiku kutwa usielewe ukaelewa subuhi. Yes! Umelipa gharama.
Mungu akubariki sana na sambaza makala hii iwe baraka kwa mwenzako. Lakini ili imsaidie lazima alipe gharama. Lazima aende kinyume na utamaduni wa kutaka kusoma vitu vifupi vifupi. Aanze utamaduni mpya wa kulipa gharama kwa kusoma vitu virefu. Na mtihani wa kwanza na hii makala kama gazeti la Daily News-Paul R.K Mashauri
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)