MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
RIWAYA NA HADITHI FUPI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
RIWAYA NA HADITHI FUPI
#1
DARASA LA RIWAYA YA KISWAHILI 
Kozi hii itajumuisha saa 3 za kujifunza kwa juma, ambapo saa 2 ni za mhadhara na saa 1 ya semina. Majuma 15 ya ufundishaji pamoja na majuma 2 ya mitihani ya chuo yatatumika kukamilisha ujifunzaji na ufundishaji wa kozi hii.
Maelezo ya msingi juu ya kozi hii
Kozi hii inalenga kutoa taaluma kunt‘u juu ya riwaya ya kiswahili kwa kuangazia chanzo na maendeleo ya riwaya sambamba na ufafanuzi wa vipera vyake. Vilevile inajadili athari zitokanazo na kuwepo kwa riwaya ndani ya jamii, mwisho, inaangazia vijenzi muhimu katika masimulizi ya kubuni.
Malengo ya kozi
Kozi hii itawawezesha wanafunzi kuuchunguza na kuutathmini muundo wa nje na wa ndani wa taaluma nzima ya riwaya ya kiswahili na riwaya zenyewe za kiswahili. 
 MUHTASARI WA KOZI
1.   Nadharia ya riwaya:
· Dhana ya riwaya
· Historia ya chimbuko la riwaya
o   Riwaya na matapo ya fasihi
o   Dhana ya ubunilizi katika riwaya
o   Muundo wa riwaya
o   Mikondo (aina) kuu za riwaya
2.   Riwaya ya kiswahili
·        Maana ya riwaya ya Kiswahili
·        Historia ya riwaya ya Kiswahilio   Kabla ya uhuruo   Baada ya uhuru
o   Kipindi cha kuanzia miaka ya 1980
o   Baada ya kutamalaki kwa zama za sayansi ya teknolojia
·        Maendeleo ya riwaya ya Kiswahili (Sababu za kuibuka, kukua na keenea ama kudumaa kwa riwaya ya Kiswahili).
·        Wanariwaya maarufu wa riwaya ya Kiswahili
3. Mbinu za kifani zinazotumika katika ujenzi wa riwaya za Kiswahili
o   Naratolojia (Usimulizi, mwendo)
o   Msuko wa vitushi na motifu zake
o   Uhusika na wahusika
o   Mtagusano wa kifasihi
o   Matumizi ya lugha
o   Mianzo na miisho ya kifomula
4. Mitazamo na mielekeo inayojichomoza katika riwaya za Kiswahili
o   Dhana ya usomaji wa riwaya za Kiswahili (maana, hadhi matatizo)o   Uhai au ufu wa riwaya za Kiswahilio   Mawazo yaliyotamalaki katika riwaya ya Kiswahili katika mapito yakeo   Masuala mtambuka katika riwaya za Kiswahilio   Tathmini ya mchango wa riwaya ya Kiswahili kwa ustawi wa waswahili
5.  Uhakiki wa riwaya Teule za Kiswahili
o   Dhana ya uhakiki na nadharia za kuhakikia kazi za fasihi
o   Kuchambua riwaya teule za Kiswahili
o   Ulinganuzi na ulinganishi wa vipengele muhimu vya kiuhakiki vijitokezavyo katika       riwaya za Kiswahili
      Riwaya Teule zitakazoshughulikiwa:
o   Nagona
o   Kusadikika
o   Kasiri ya Mwinyi Fuad
o   Mfadhili
o   Barua Ndefu kama hiio   Mirathi ya Hatari
o   Bwana Myombekele na Bibi Bugonoka
o   Hofuo   Pesa zako zinanuka
o   Mzimu wa watu wakale
         Namna ya Ufundishaji: 
Mihadhara na Mijadala.
         Saa za Ufundishaji: 
Jumla ya saa 45, saa 30 za Mihadhara na 15 za  Mijadala.
         Upimaji: 
Alama za Tamrini 40% na Mitihani ya mwisho 60%.
       
MATINI ILIYOTUMIKA 
Nadharia ya Riwaya
Kumekuwa na misuguano kadhaa kutoka kwa wanazuoni waliothubutu kutoa fasili ya riwaya. Imeonekana wazi kuwa kunakukubaliana kwa baadhi ya masuala na kutofautiana pia katika kutoa fasili hii. Miongoni mwa masuala yaliyopelekea misuguano katika utoaji wa fasili hii ni pamoja na:o   Dhima / maudhui ya riwayao   Mipaka ya riwaya pindi inapohusishwa na hadithi fupi au novelao   Ukubwa / urefu wa riwayao   Aina za riwaya
Kuna wengine huchanganya utanzu wa riwaya na vijitanzu vingine vya kinathari (yaani, vile vitumiavyo lugha ya mjazo) kama vile Hadithi fupi, Novela, Tawasifu na Wasifu.
Hadithi fupi
Tofauti yake na riwaya hujikita katika upeo na uchangamani. Hii inamaana kuwa hadithi fupi huwa sahili sana ilihali riwaya huwa imetanza zaidi.
Novela
Hii huwa ni changamani zaidi kuliko hadithi fupi. Huweza kuwa na visa vingi kiasi kulinganisha na hadithi fupi.
Tawasifu
Ni utungo utumiao lugha ya mjazo ukisimulia habari za mtunzi mwenyewe.
Wasifu
Ni utungo utumiao lugha ya mjazo ambapo mtunzi husimulia habari za mtu mwingine.
Ukichunguza kwa makini vijitanzu hivyo utaona kuwa vinatofautiana na riwaya katika vigezo vya: urefu, uchangamani, idadi ya wahusika, lugha, vitushi, U―Kina, dhamira n.k.
Hivyo, mtu anayetaka kuifasili dhana ya riwaya hupaswa kumakinika katika vipengele hivyo.
Maswali ya msingi
1.  Wanazuoni mbalimbali wametoa fasili ya riwaya. Eleza fasili hizo.
2.   Kwa nini fasili zao zimetofautiana?
3.   Je, wewe unadhani riwaya ni nini?
4.   Eleza tofauti ya riwaya na vijitanzu vingine vya kinathari.
5. Unadhani tofauti hizo kati ya riwaya na vijitanzu vingine vya kinathari zinasababishwa na nini?
Sifa bainifu za riwaya
Ilinganishwapo na tanzu nyingine, riwaya huwa nasifa bainifu zifuatazo:
o   Kutokufungwa na sheria nyingi (kinyume na makumbo mengine ya tamthiliya na ushairi).
o   Matumizi ya lugha ya kinathari.
o   Kuwa na mawanda mapana katika urefu na kina.o   Ni zao halisi la kibepari.
o   Kuwa na uhalisi kwa kiasi kikubwa.
o   Mahitaji ya kusoma na kuandika.
o   Kuwepo kwa maisha na makazi yenye utulivu.
o   Kuwa na uwezo wa kugusia hadi vitu vionekanavyo kama vidogo (kwa maelezo       zaidi, tazama. Madumulla, 2009).
Miega ya Riwaya
Mwega ni nguzo au kiunzi kitumikacho kushikilia jambo / kitu. Kama ilivyo kwa kila kazi ya fasihi, riwaya yoyote lazima ijiegemeze katika miega au nguzo tatu muhimu za muktadha, fani na maudhui. Miega hiyo huishikilia vema riwaya katika uundwaji pamoja na utumiwaji (usomaji na uhakiki) wake. Miega yenyewe ni hii ifuatayo:
Muktadha                                                      
Muktadha ni kitu cha lazima katika kila riwaya kwasababu ndiyo huipa uhai riwaya yoyote. Riwaya yoyote hutokana na muktadha fulani au mseto wa miktadha kadhaa. Aghalabu, miega mingi ya fani na maudhui hujengwa kutoka katika nguzo hii. Hivyo, ni lazima riwaya iiakisi miktadha hiyo. Aghalabu, ni nadra sana kukuta riwaya imejikita katika muktadha wa namna moja pekee. Kwa hiyo, riwaya nyingi ni zao la mseto wa miktadha ambayo mtunzi huipitia.
Tanbihi: dhana hii ya muktadha ni vema ikachukuliwa kwa upana wake. Wengi huifinya kwa kuinasibisha na mazingira ya kijiografia (mandhari) pekee! Miktadha yaweza kuwa ya:o   Taarifa za msingi zinazomuhusu mtunzi (kuzaliwa, kazi, elimu n.k)o   Jografia (mandhari) ya maisha na mapitoo   Historia ya mapito yake / jamii yake (matukio muhimu yaliyomgusa yeye au jamii yake)o   Utamadunio   Uchumi n.k.
MAUDHUI
Nayo ni nguzo muhimu sana. Bila maudhui, hakuna riwaya. Hivyo, kila riwaya iliyosanwa vema lazima iwe na mwega huu. Ndani ya maudhui kuna mambo muhimu matatu ambayo ni: ujumbe, dhamira na vipopo vya fikra.
Dhamira
Baadhi ya wataalamu hudai kuwa dhamira muhimu zipo 4: nazo ni: kuburudisha, kuhifadhi amali na historia, kuelimisha na kupambana na maovu / madhila yaikumbayo au yatakayoikumba jamii.
Vipopo vya Fikra
Vipopo vya fikra au vitumba vya mawazo ni mawazo yajengekayo katika akili ya msomaji au mhakiki kutokana na vitushi vya riwaya, aghalabu, hutokana na utambuzi wake binafsi kuhusu mambo mbalimbali au tajiriba. Wengine huviita dhamira ndogo ndogo. Mara nyingine, vipopo vya fikra siyo lazima vijioneshe moja kwa moja riwayani. Bali, msomaji au mhakiki huweza kujiwa navyo tu kadri asomavyo riwaya huku akihusisha na utambuzi wake binafsi au tajiriba.
Ujumbe
Haya ni mavuno ayapatayo msomaji kutokana na dhamira au vipopo vya fikra. Pia, si lazima ujumbe aupatao msomaji au mhakiki ulandane na kile alichokikusudia msanii. Hii ni kwasababu, msomaji au mhakiki huweza kujenga maana ya akisomacho kutokana na kuhusisha na mazoea na utambuzi wake binafsi.
FANI
Huhusisha vipengele vitengenezavyo umbo na sura ya riwaya (mjengeko na ladha ya riwaya). Vipengele hivyo viko katika makundi mawili ya: Muundo na Ubunilizi.
Dhana ya Muundo katika Riwaya
Hii hurejelea mjengo wa kazi yenyewe. Hujumuisha vipengele mbalimbali ambavyo huiweka kazi katika umbo na muundo husika. Muundo wa kazi ya mwandishi wategemea zaidi kanuni asilia za kazi husika pamoja na jamii aiandikiayo. Ili kupata mjengeko autakao katika kazi yake, msanii hutumia mbinu mbalimbali. Mbinu hizo huhusisha vipengele kama vile:
i.      Mtindo                                  
ii.   Lugha
iii.    Vitushi                                  
vi. Migogoro
v.  Udhamira                            
vi. Muwalai
vi.     Wahusika                            
vii Mandhariv.                 
Ushikamani                                                      
Mitindo mbalimbali ya utunzi na uandishi hutokana na athari malimbali za jamii ambayo mtunzi amekulia au vionjo binafsi vya mtunzi.Kipengele kingine katika suala la mtindo ni matumizi ya nafsi. Dhana hii ya matumizi ya nafsi hurejelea matumizi ya midomo ya wahusika katika kufikisha mwazo yake. Waandishi wengi hupendelea nafsi I na ya III. Nafsi II haitumiki kwa sababu humrejelea msomaji. Hivyo, waandishi huepuka kumchoma na kumchusha msomaji. Nafsi I na III zina uhuru wa kuzitumia kwa sababu hujiweka mbali na athari zozote zimwelekeazo msomaji. Suala la nafsi ni muhimu sana katika uandishi. Kwa jumla, mbinu za kimuundo ni kipengele cha lazima cha mwega huu wa fani. Kamwe, hakiwezi kukosekana katika kazi husika na kazi hiyo ikabaki kuwa katika utanzu husika. Kipengele hiki ni tofauti na kipengele cha mbinu za kibunilizi.
Dhana ya Ubunilizi katika RiwayaRiwaya, pamoja na kazi za tanzu nyingine kama vile nudhumu na tamthiliya ni kazi za kibunilizi. Neno Ubunilizi au Ubunifu linatokana na kitenzi buni. Kubuni ni kuunda jambo. Aghalabu, jambo hilo huwa katika hali ya kidhahania kabla halijaonekana au halijadhihirika kwa hadhira kupitia ogani za fahamu. Hivyo, kwa jumla, twaweza kusema kuwa ubunilizi ni uwazaji na uundaji wa wazo katika hali inayohalisika. Dhana ya ubunilizi hutusaidia kutofautisha fasihi na matukio halisi maishani. Fasihi si maisha halisi bali ni tokeo la ubunifu wa mtunzi yaani, mtunzi ana uwezo wa kubuni visa na wahusika wake kwa njia ambayo haikanganyi hali halisi ya maisha. Mambo muhimu yamwezeshayo mtu kutunga kazi bunilizi ni:
o   Silika / karama / kipawa
o   Uwezo wa kiutafiti
o   Uzoefu
o   Mawazo au fikra (taaluma)
o   Nia, lengo au azma
Misingi hii yatudokezea na kutusaidia kujibu swali la msingi tupaswalo kujiuliza tuifikiriapo kazi fulani ya kibunilizi na kuichukulia kuwa bora/nzuri ni: je, kazi hiyo ni tokeo/zao la msingi ya kitaaluma? Au silika (kipawa/karama)? Au tajiriba (uzoefu wa kimaisha)? Au ni tokeo la mseto wa vipengele hivyo vyote? Au ni tokeo la mseto wa baadhi ya vipengele hivyo?
Ubunifu wa riwaya na bunilizi za tanzu nyingine lazima uongozwe na kaida mbalimbali za hali halisi ya maisha. Mtunzi anapaswa kuufanya ulimwengu wake wa kubuni kuwa picha halisi ya maisha katika ukamilifu na ukweli wake. Uhalisia ni ukweli wa jambo kama lilivyo au linavyofahamika. Kuna ukweli wa aina 2 ambazo ni:
o   Ukweli katika hali halisi (uhalisi na uasilia wa jambo/kitu).
o   Ukweli wa kisanaa (husawiri mambo yaliyobuniwa na mtunzi).Hivyo, ubunilizi ni utengenezaji wa ukweli wa jambo kadri afikiriavyo na akusudiavyo msanii. Kwa jumla, msanii hufanya ubunilizi kwa kuzingatia vigezo muhimu vinne. Hivi ni:
o   Kaida za jamii (yake au anayoiandikia)
o   Uwezekano wa utokeaji wa jambo husika
o   Azma au lengo (hisia? ufunuo? kujibu?)
o   Hadhira 
Yafaa ubunilizi usipitilize, kwani ni rahisi kwenda mbali na jamii halisi inayoandikiwa. Hata hivyo, ifahamike kuwa kumtaka mtunzi afuate kaida fulani si kumnyima uhuru wa ubunifu. Kama mtunzi atakanganya hali halisi ya maisha kama mbinu yake ya kutunga, basi na tumpe uhuru huo ilimradi kazi yake twaielewa kwa mtizamo huo. Kazi yoyote ya kisanaa lazima iwe na vipengele muhimu vya aina/makundi mawili. Haya ni: vipengele vya kimuundo na vipengele vya kibunilizi.
Vipengele vya kimuundoHivi ni vile vinavyoifanya kazi husika iwe katika utanzu au kumbo husika. Kila utanzu una aina na namna zake za vipengele vya kimuundo. Vipengele hivyo ndivyo huwa nguzo―msingi zishikiliazo tanzu husika. Kazi fulani hujulikana kuwa ni aina ama shairi, utenzi, utendi, hadithi, fupi, riwaya au tamthiliya kutokana na vipengele hivi. Vipengele vya kimuundo hutegemeana na utanzu husika. Hata hivyo, aghalabu, huhusisha vipengele kama vile: vitushi, uhusika na wahusika, ushikamani, lugha, muwala na mandhari.
Vipengele vya kibuniliziNi jumla ya mambo ambayo mtunzi huyabuni na kuyaingiza au kuyatumia katika kazi zake ili ilete mvuto na mnato kwa hadhira. Mbinu hizi huakisi kipawa cha utunzi alichonacho mtunzi na kumtofautisha na watunzi wengine. Hii ni kwa sababu, kupitia mbinu hizo, kazi hubeba vionjo tofauti (hata kama kazi hizo tofauti zinazungumzia jambo au mada inayofanana, lazima zitatofautiana kutokana na matumizi ya mbinu tofauti za kibunilizi). Vipengele vya kibunilizi vitumiwavyo sana na watunzi wa riwaya za Kiswahili ni:
i.    Taharuki                         
ii. Kisengerenyuma
iii.  Utomeleaji                    
vi.Ufumbaji
v. Ritifaa                           
vi.Usawiri wa wahusikai
vii.  Dayolojia                      
 viii. Utanzia
xi.  Ujadi                                
x.  Ufutuhi
Taharuki Ni hali ya kuwa na dukuduku la kutaka kujua juu ya nini kitafuatia katika usimulizi wa kazi ya fasihi. Mtunzi huijengea hamu hadhira yake ya kutaka kujua zaidi. Mbinu hii hutumiwa sana/hujitokeza sana katika kazi za fasihi pendwa. Hujitokeza pia katika fasihi nenwa. Taharuki, katika kazi za fasihi simulizi hujengwa kwa kutumia:
o   Mabadiliko ya lugha―uso/sura
o   Vipashio vya fonolojia arudhi
o   MatendoNa, katika fasihi andishi, taharuki hujengwa kwa kutumia:
o   Mbinu nyingine za kibunilizi k.v. kisengerenyuma
o   Utumizi wa wahusika wa ajabu―ajabu
o   Mandhari ya ajabuajabu
Kisengerenyuma Ni namna ya kupangilia vitushi au kusimulia kwa kuanza na tukio―tokeo kisha kufuatia tukio―chanzi. Watunzi huitumia kwa namna tofautitofauti. Mbinu hii pia husaidia sana kuboresha hamu ya hadhira kutaka kujua muundo wa vitushi vya kazi husika.
UtomeleajiHujulikana pia kama mwingiliano wa tanzu. Ni kitendo cha kuchopeka/kuingiza vipande vya utanzu mwingine (ulio tofauti na utanzu ushughulikiwao) na katika utanzu mkuu ambao mtunzi anautunga. Kwa mfano, mtunzi wa hadithi fupi huweza kuchopeka mashairi/tenzi au barua katika kazi yake kuu. Utanzu wa nathari huongoza kwa uhuru wa kufanya utomelezi ulinganishwapo na tanzu nyingine. Mbinu hii huwa na tija zifuatazo:
o   Kuonesha umbuji wa tanzu hizo
o   Kuimarisha maudhui
o Kuondoa uchovu kwa wasomaji
o   Kuweka msisitizo
o   Kujikaribisha na uhalisi (senkoro, 2011:70―71).
UfumbajiNi utumiaji wa kauli zenye maana fiche. Kauli hizo huwa na maana iliyo kinyume au tofauti na umbo la nje la kazi au matini husika. Ufumbaji huweza kujitokeza katika: Anuani/mada/kichwa cha habari, majina ya wahusika, Aya, Sura ya kazi, kazi nzima n.k. tija zake ni:
o   Kuonesha umbuji wa kisanaao   Kuishirikisha hadhira kwa karibu
o   Kujitanibu na ghasia za kufuatwa―fuatwa na mkono wa dola.
UjadiHuu ni utumiaji wa kauli, matendo au mazingira ya asili yanayofungamana sana na jamii inayoandikiwa. Aghalabu, ujadi hujumuisha:o   Kauli kama vile methali, nahau, vipengele mbalimbali vya kimazungumzo ambavyo hutumiwa sana na jamii husika.o   Matambikoo   Vyakula asiliao   Watunzi hufanya hivyo ili kujiweka karibu na hadhira yao.o   Yaani, hadhira hujiona iko karibu sana na kazi husika waonapo baadhi ya vipengele vya usimulizi na kiutendaji vya kijadi wavitumiavyo kila siku vimetumiwa katika kazi fulani ya fasihi.
o   Pengine, husaidia kuongeza au kupanua hadhira.
DayalojiaHii ni mbinu ambayo mtunzi hutumia kauli za majibizano katika kuwasilisha mawazo yake. Hutumia vinywa vya wahusika wake kudokeza maudhui ayalengayo. Katika baadhi ya tanzu, dayalojia huwa ni kipengele cha kimuundo (kwa mfano, tamthiliya dayalojia ndiyo kijenzi cha msingi cha utanzu huu husika). Na kwa tanzu nyingine hujitokeza kama kipengele cha kibunilizi. Tija zake ni:
o Huondoa uchovu kwa wasomaji
o Huonesha ufundi wa mtunzi katika matendo, maneno na hadhi ya                                    wahusika.
o Husaidia kuwasilisha mawazo kwa hali ya uasili (mtunzi huwa mbali na                       uwasilishaji, hadhira hupata ladha ya maudhui kutoka kinywa asilia).
Usawiri wa wahusikaNi kitendo cha kuwachora, kuwafafanua, kuwatambulisha na kuwajenga wahusika huku wakipewa maneno, matendo, hadhi na uwezo unaolandana au unaowiana na uhusika wao. Wahusika hutumia mbinu nyingi sana katika kuwasawiri wahusika katika kazi zao. Mbinu hizo ni:
o   Majazi: utoaji wa majina kulingana na sifa, tabia au dhima. Kwa mfano,             Rosa Mistika (katika Rosa Mistika) na Sulubu (katika Nyota ya Rehema).
o   Uzungumzaji nafsi
o   Kuzungumza na hadhirao   Kuwatumia wahusika wengine (Mhusika 1                 kumfafanua mwingine).
o   Ulinganifu wa usambamba
o   Maelezo (mtunzi kumwelezea mhusika)
RitifaaNi hali ambayo mtu mmoja hufanya mawasiliano na mtu aliye mbali naye (umbali huo huweza kuwa wa kijiografia au kufariki). Aghalabu, mawazo yasawiriwayo kupitia mbinu ya ritifaa huwa na vionjo vya kihisia sana. (kila mmoja kwa wakati wake achunguze ujitokeaji wa ritifaa katika riwaya zilizoteuliwa kama zilivyoainishwa kweye muktasari wa kozi hii).
UfutuhiNi mbinu ambayo mtunzi hutumia vipengele mbalimbali vizuavyo ucheshi, raha, kicheko au furaha kwa hadhira yake. Vipengele hivyo huweza kujengwa na kejeli, utani, dhihaka, ubeuzi na mizaha. Miongozi mwa tija zake ni:o   Kufurahisha hadhirao   Kuwaondolea uchovuo   Kujikwepesha na nguvu za dolao   Kulainisha uwasilishaji wa maudhui yanayochoma au yenye hisia kali (utasifida).
UtanziaMbinu hii ni kinyume cha ufutuhi. Ni mbinu ambayo mtunzi hutumia vipengele mbalimbali vizuavyo huzuni, masikitiko, jitimai na mateso kwa hadhira yake. Vipengele hivyo huweza kujengwa na: mateso, ugumu wa maisha, vifungo, mabaa kama vile njaa, gharika, kimbunga, magonjwa na ulemavu (wa viungo au michakato ya mwili kama vile ugumba na utasa).
HISTORIA YA RIWAYA
Riwaya na Matapo ya Fasihi
Matapo ni vipindi mbalimbali vya kihistoria ambavyo fasihi au sanaa kwa jumla imevipitia. Matapo pia huweza kutafsiriwa kuwa ni mkondo au makundi makuu ya kinadharia ambayo yametawala katika fasihi/sanaa katika nyakati maalumu. sanaa/fasihi imepitia katika mikondo mingi sana. Bali ile mikuu ni minne. Nayo ni:
o   Tapo la Urasimi Mkongwe (850 ― 325 K. Y. M)
o   Tapo la Urasimi Mpya (1680 ― 1780 B. Y. M)
o   Tapo la Ulimbwende (1790 ― 1870 B. Y. M)
o   Tapo la Uhalisia (Baada ya utawala wa Malkia Viktoria na Mapinduzi ya viwanda hadi sasa).
Matapo haya yaliingiliana na kukamilisha kwa kiwango kikubwa katika muda wa kuwapo kwake. Hivyo, yawezekana kuwa matapo mawili au zaidi yakatamalaki kwa wakati mmoja.
TAPO LA URASIMI MKONGWE
Dhana ya Urasimi humaanisha mkusanyo wa mikondo ya kifikra au kimtazamo ambayo chanzo chake ni sanaa na utamaduni wa Wayunani na Warumi. Dhana hii ilijiegemeza sana katika usimikwaji wa sheria na taratibu mbalimbali za kuongoza utendekaji wa sanaa/fasihi. Sehemu kubwa ya mawazo yao katika sanaa ilimezwa na nadharia ya MWIGO. waasisi/wadau wakuu wa Urasimi mkongwe ni: Plato na Aristotle
Muhtasari wa Mawazo ya Plato Kuhusu Sanaa
o Uhusiano baina ya uwezo wa mshairi na nguvu za Mungu. Anaamini kuwa msanii ni kiumbe kitakatifu ambach
o hupokea mawazo maalumu/ufunuo kutoka kwa Mungu ili afikishe ujumbe kwa hadhira.
o Uwezo wa msanii hautokani na hekima zake, bali jazba na mpagao utokao kwa Mungu.
o Muigo si chochote, kwani msanii huigiza uhalisia wa maisha ambao hata yeye mwenyewe haujui.
o Alitoa sheria muhimu zilizopaswa kuimiliki sanaa ya utungaji mashairi (wasanii wote walipaswa kuzifuata). Sheria hizo ni:
o Kazi yoyote ya ushairi lazima ipitiwe na kamati maalumu ya watu wenye umri wa zaidi ya miaka 50.
o Watunga mashairi wote lazima watimize miaka 50.
o Ushairi lazima ueleze mazuri tu (kama vile juu ya mashujaa na watawala wa nchi).
o Washairi wasitunge chochote kilicho kinyume cha sheria za Jamhuri. (Rejea kitabu chake, The Laws)
Muhtasari wa Mawazo ya Aristotle juu ya Sanaa
o Kuhusu Ushairi na Tamthiliya (sanaa): Mwigo/uwakilishi ni nadharia bora. Kulingana na Aristotle, mwigo ni kiwakilishi cha maisha (uhalisi), maisha yenyewe halisi. Mwigo hupunguza au kuondoa madhara yatokanayo na woga au hasira.
o Kuhusu Hadhira: Sanaa iwe na hadhira mbili ambazo ni: Hadhira ya watu wa nasaba bora (Tanzia) na Hadhira ya watu wa nasaba duni (Futui). Tanzia: kwa mujibu wa Aristotle, ni masuala tata yenye kusikitisha na kufikirisha. Futuhi: ni masuala mepesi na yanayochekesha. Watu duni wapewe haya kwa vile akili yao haiwezi kuchambua mambo.
o Kuhusu Muundo mahususi: Sehemu za kazi ya sanaa sharti zioane/ziwiane. Kazi ya sanaa iwe na sehemu 3 ambazo ni kichwa, kiwiliwili na miguu. Miundo hii itofautiane kulingana na aina ya kazi (kama ni tanzia au futuhi). Alisisitiza kuwapo kwa nguzo muhimu katika sanaa (tamthiliya). 
Nazo ni:
ü Muundo/msuko
ü Wahusika
ü Nyimbo
ü Wazo kuu (maudhui)
ü Hadhira
ü Lugha bora kulingana na hadhira
oKuhusu Historian na ukweli katika sanaa: Sanaa ni mwigo au kiwakilisho cha ukweli na uhalisia wa maisha ya jamii. Hivyo, mwanasanaa huelezea historia kupitia sanaa. Huweza kuweka mipaka ya historia iliyopita na iliyopo. Pia huweza kuvuka mawanda ya uhalisia uliopita na uliopo. Hivyo akasema Sanaa ni halisi kuliko uhalisi wenyewe. Na ina ukweli zaidi kuliko ukweli wenyewe.
Vigezo vya Jumla vya Tapo la Urasimi
o   Kuwapo kwa fani mahsusi
o   Kuoana kwa fani na lengo/maudhui ya kazi ya sanaa (ulinganifu)
o   Kueleweka kwa kazi ya sanaa (urahisi)
o   Kutiliwa maanani kwa muundo na mpango mahususi
o   Mtindo mahsusio   Kuheshimu jadi
o   Kutotawaliwa na jazba (msanii aitawale jazba).
TAPO LA URASIMI MPYABaadhi ya wadau wake ni: Donne, Market, Herrick, Hrbvert, Cowley, Vongham, Crasha na wengine wengi.
Mambo ya Msingi Kuhusu Tapo hili ni:
o   Lilizingatia kigezo cha Mantiki na Mjadala katika kazi za sanaa (mashairi)
o   Kazi za sanaa lazima ziwe na fumbo litakalomfikirisha msomaji (hadhira)
o   Sanaa lazima iwe kwa ajili ya watu. 
Wadau wa tapo hili walimchukulia binadamu kuwa ni kiumbe mwenye kasoro asotimia; ambaye alitakiwa arekebishwe na kazi za fasihi/sanaa. Hivyo, kufaulu au kushindwa kwa kazi ya fasihi/sanaa kupimwe kulingana na kufaulu au kushindwa kwake kumzingatia/kumtumikia mtu. Yaani, sanaa lazima imfurahishe, imsahihishe na imwelimishe mtu katika maisha yake.
o   Kuwapo kwa Mpango mahsusi katika kazi ya sanaa.
o   Kuzingatiwa kwa sheria za utungaji kulingana na aina ya utanzu.
Athari za Tapo la Urasimi Mpya katika Sanaa ya sasa
o   Uteuzi mahsusi wa maneno na tungo/mishororoo   Umuhimu wa taswira katika ushairio   Matumizi ya akili kuliko jazba (hasa wakati wa utungaji wa kazi za fasihi)
TAPO LA ULIMBWENDELilishamiri barani Ulaya mnamo karne ya 18 hadi 19. Lilitokana na msisimko wa kifasihi, kifalsafa, kidini, kisiasa  na kisanaa kutokana na Urasimi mpya. Wadau maarufu wa Tapo hili ni:
o Uingereza, walikuwa: William Wordsmith na George Grabbe
o Ujerumani, walikuwa: Goethe, Holderline na Schiller
o Ufaransa: Victor Hugo
o Italia: Novalis
Mambo ya Msingi kuhusu Tapo hili:
o  Sifa yake kuu ni uhuru wa msanii. Msanii alipata uhuru wa kuchagua mada, hadhira na lugha kwa matakwa yake. Mambo ya kufikirika kama vile mambo ya ndoto/ruya yalianza kuandikwa.
o Pia wahusika wa ajabuajabu walianza kutumika kwa mfano, shetani na jangili.o   Lilizingatia hisia za ndani pamoja na mazingira ya mzungukayo mtu huyo.
o Tapo hili lilielezea maisha jinsi wao (watunzi) walivyotaka yawe.Kuzuka kwa tapo hili kulichangizwa na kuwapo kwa mambo kadhaa ambayo yalisababisha msisimko na athari za maisha ya wakati huo. Mambo hayo ni:
o  Safari za kuvumbua ulimwengu
o   Harakati za USA kudai uhuru wakati huo
o   Kuzuka kwa miji na viwanda kwa haraka
o   Ulinganishi wa nguvu za kisilaha na kisiasa baina ya mataifa mbalimbali
o   Mivutano na harakati za kitabaka.
Vigezo vya Jumla vya wana―Ulimbwende ni:
o   Kutilia mkazo mazingira na asili
o   Kuandika/kusana kazi mbalimbali zilizowazungumzia wahusika kuanzia utoto waoo   Matumizi ya wahusika wa ajabuajabu kama vile shetani, jangili, wavunja sheria, Malaya n.k.
o Kuruhusu matumizi ya ndoto zilizovuka mipaka ya uhalisi wa maisha. Hii iliruhusiwa ili kurekebisha matumizi ya fani na maudhui katika utunzi.
o Kupinga sheria zilizowekwa na Wanaurasimi: kama vile: Kutenga hadhira, kutenga mitindo ya lugha kulingana na matabaka ya hadhira na kutenga baadhi ya wahusika kulingana na nasaba.
TAPO LA UHALISIA
Uhalisia ni sawa kabisa na udodosi―mambo ambapo huwa na uzingatiaji mkubwa wa uhalisi katika kuwasilisha uhalisi huo katika fasihi. Lilielezea maisha kwa jinsi yalivyo, yaani jambo lilielezwa kwa undani na kweli. Miongoni mwa waasisi wake ni Hegel. Mazingira na wahusika walisawiri kikwelikweli kuyaakisi maisha ya kila siku (kwa kuzingatia furaha, huzuni, matumaini, matazamio na matatizo)Lilishamiri katika karne ya 20. Tapo hili lilijihusisha sana na riwaya. 
Mambo yaliyochochea kuzuka kwa Tapo hili
o   Maendeleo ya sayansi na teknolojia
o   Kuwepo kwa silaha kali na mapigano
o Mivutano au migogoro kati ya matajiri na maskini duniani kote
o  Vuguvugu la nchi nyingine kudai uhuru
Vigezo vya Tapo la Uhalisia
o   Demokrasia katika uumbaji wa fani na maudhui ya kazi ya fasihi
o  Usawiri mwanana wa mambo yanayotokea kila siku katika maisha ya watu.
o   Kuijua kwa kina dhana ya MWIGO. Mwanauhalisia lazima ajue jinsi ya kuiga na akijue akiigacho. Kwa kufanya hivyo, itasaidia nafasi kati ya kiingwacho na mwigo kutokuwa kubwa.
o Kutofungwa na ulazima wa kuwa na mpangilio wala muundo maalum katika kazi za sanaa. Hii ni kwa sababu maisha hayana muundo wala mpangilio maalum.
o Msanii azingatie athari za kazi yake katika hadhira yake.
o Athari hizo zaweza kuletwa na mambo kama vile urahisi (au usahili katika usanaji), umoja kwa moja katika kufafanua maudhui na usahihi wa mambo.
o Kazi yoyote ya fasihi lazima iwe na jukumu la kuadilisha na kufunza.
Aina za uhalisia
1.     Uhalisia wa Kibwanyenye
2.     Uhalisia wa Kihakiki
3.     Uhalisia wa Kijamaa
4.     Uhalisia Ajabu
Uhalisia wa Kibwanyenye
Waandishi wake huandika na kusawiri uozo wakati wa ubwanyenye. Hata hivyo, hawatoi masuluhisho ya kisayansi kuhusu migogoro iliyomo katika jamii.
Uhalisia wa Kihakiki
Mawanda yake hayaivuki jamii husika. Huihakiki jamii hiyo husika tu. Huchambua mambo ya jamii kwa namna moja, kwandani tu au kwa nje tu.
Uhalisia wa Kijamaa
Huchambua mambo ya jamii kutoka ndani na nje ya jamii. Humchambua mhusika kwa kumhusisha na nguvu mbalimbali za kijamii, kiuchumi, kiutamaduni na kisiasa.
Uhalisia Ajabu
Wengine huuita uhalisia mazingaombwe. Huchanganya uhalisia na mambo ya ajabuajabu. Uajabu―ajabu hapa unarejelea matumizi ya wahusika, mandhari na hata vitushi vilivyo nje ya hali ya kawaida. Mfano mmojawapo wa kazi iliyo katika kijitapo hiki ni Baba alipofufuka, utata wa 9/12, Nagona n.k.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)