MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JE, WAFAHAMU AINA ZA HARUSI YA KISWAHILI?

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
JE, WAFAHAMU AINA ZA HARUSI YA KISWAHILI?
#1
JE, WAFAHAMU AINA ZA HARUSI YA KISWAHILI?
Ameandika Haayati Shaaban Robert katika Insha yake “ARUSI YA KISWAHILI” katika kitabu kiitwacho “KIELELEZO CHA INSHA” Harusi zijulikanazo ni saba, nazo ni;

1. Ya Kuhala
2. Ya Mti
3. Ya Kigumbu
4. Ya Lima
5. Ya Sahani
6. Ya Kombe
7. Ya Kilili.”
 
NIKUFAFANULIE TOFAUTI ZAKE BAINA YA HARUSI MOJA NA NYINGINE;
Haayati Shaaban Robert akitaja ufafanuzi wa harusi hizo saba kaonesha kuwa zinatofautiana katika kuzisherehekea kwake. Basi kama umeshaingia ndoani tazama hapa ujuwe ulifanya harusi gani ya Kiswahili, na kama bado, utaamua sasa wakati ukifika wataka fanya harusi gani kati ya hizi?

1. Kuhala- “Hii ni ile Arusi ambayo haiadhimishwi.”
Yaani ikishapita ndoa basi ndo imekwisha. Hakuna tena kumbukumbu ya miaka mingapi sijuwi ya ndoa yetu wala nini. (Ufafanuzi wangu)
 
2. Mti- “Hii ni Arusi ambayo haina sherehe” kabisa yani. Kimya kimya. Kwa uzoefu wangu zinakuwa za kuongeza mke wa pili, n.k. Au zile tuitazoa za mkeka, hakuna vifijo labda vya kimbea tu. (Ufafanuzi wangu).

3. Kigumbu- “Hii ni ya karamu ndogo tu”.
Hapa hakimwagiki kipunga wala. Hata watoto wa Uswahilini hawambulii kitu hapa. Hustuliwa wale watu muhimu muhimu sana tu.(Ufafanuzi wangu)
 
4. Lima-” Hii ina karamu kuuubwa” Yaani hapa ndo hata watoto wa Uswahilini twakimbia na kipunga mikononi au chochote kilichoandaliwa. Humu ndimo wazee wetu wanaweza rudi na mifuko. Karamu kubwa.
5. Ya Sahani. “Hii hufuatwa na karamu ya juma moja”
Juma si kama tunavyofasiri sisi ati siku moja. Juma/jumaa ni wiki au siku saba karamu yaliwa tu. Wiki nzima watu wapishana, vyakula kwa vinywaji humwagika (Ufafanuzi wangu)
BWANA WEE! AYAJUWE NANI HAYA KAMA SI SISI WENYEWE WASWAHILI? NASEMA WASWAHILI NDO SIYE.
6.Kombe- “Hii ni harusi ambayo huandaliwa karamu ya jamaa/wiki mbili, yaani watu washereheka tu kwa kula na kunywa.
7. Kilili- “Hii ni ya mwisho ambayo huandaliw karamu ya mwezi mzima na fungate kubwa.
“Waswahili wenyewe hupenda harusi nne za mwisho. Harusi hizi ni Maarufu sana kwa fakhari na adhama zake. Hazimaliziki kwa siku moja. Zina matengenezo makubwa. Washoni na masonara huajiriwa kwa kazi hii. Taarifa za makaribisho hutangulia kupelekwa. Nyumba husafikiwa. Na kupakwa chokaa hasa kwa wakati huu. Ndugu na marafiki huja toka kila mahali kama wageni. Hata katika NYUMBA YA MASIKINI KABISA kuna shughuli ya mchana na usiku kwa muda wa siku chache kabla ya siku ya arusi” UK. 73-74.
KAKWAMBIA NANI, ATI WASWAHILI TUNA DOGO?HATA TUWE MASIKINI.

***Imeandikwa na, MUDHIHIRI NJONJOLO (BABA UTENZI, MSWAHILI DHAHIRI, EL- LUGHAWIY)
MTWARA-MJINI.
0714-821926.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)