MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA MANENO ' BAHATI' NA 'HADHI - Printable Version
JIFUNZE KISWAHILI
ETIMOLOJIA YA MANENO ' BAHATI' NA 'HADHI - Printable Version

+- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz)
+-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1)
+--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16)
+--- Thread: ETIMOLOJIA YA MANENO ' BAHATI' NA 'HADHI (/showthread.php?tid=1920)



ETIMOLOJIA YA MANENO ' BAHATI' NA 'HADHI - MwlMaeda - 01-02-2022

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO ' BAHATI' NA 'HADHI'

Neno *bahati*[ *Ngeli: i-/zi-]* katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana ya' mafanikio yanayotokea kwa mtu bila ya kutarajia.

*Kuna methali:* *Asiye na bahati habahatiki*: mtu ambaye hajapangiwa kupata bahati, hawezi kuipata.

*Kuna msemo: Maisha ni bahati ifumbate*: jitahidi kufanya mambo ya maana maishani unapokuwa hai.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *bahati* (soma: *bakhtun/bakhtan/bakhtin بخت)* lina maana ya 'fursa anayoipata mtu bila ya kutarajia'. Kisawe cha neno ' *bahati* *(bakht)* katika lugha ya Kiarabu ni neno ' *hadhi* ' ( *soma: hadh-dhwun/hadh-dhwan/hadh-dhwin حظ*).

Neno *hadhi*[ *Ngeli: i-/zi-]* katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana zifuatazo:

1. Ngazi au nafasi ya heshima aliyonayo mtu katika jamii, shirika au kazi.

2. Sifa ya kumfanya mtu aheshimike na ajiheshimu.

3. Hali ya maisha ya kiwango  cha juu anayoishi mtu; maisha bora.

Katika lugha ya Kiarabu neno 'hadhi' ( *soma: hadh-dhwun/hadh-dhwan/hadh-dhwin حظ)* lina maana zifuatazo:

1. Fursa, fungu.

2. Bahati.

3. Utukufu, ubora, hali njema.

4. Mwenye bahati/fursa *dhuu hadh-dhwi ذو حظ*

Kinachodhihiri ni kuwa wakati neno *bahati* ( *soma: bakhtun/bakhtan/bakhtin  بخت*) lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa  kuwa neno *bahati* maana yake katika lugha yake ya asili - Kiarabu haikubadilika, neno ' *hadhi* ' ( *soma: hadh-dhwun/hadh-dhwan/hadh-dhwin حظ)*  ambalo ni kisawe cha neno ' *bahati* ' ( *soma: bakhtun/bakhtan/bakhtin بخت*) lilichukua dhana mpya.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*