MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA MANENO 'ABIRI' na 'ABIRIA' - Printable Version
JIFUNZE KISWAHILI
ETIMOLOJIA YA MANENO 'ABIRI' na 'ABIRIA' - Printable Version

+- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz)
+-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1)
+--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16)
+--- Thread: ETIMOLOJIA YA MANENO 'ABIRI' na 'ABIRIA' (/showthread.php?tid=1766)



ETIMOLOJIA YA MANENO 'ABIRI' na 'ABIRIA' - MwlMaeda - 12-18-2021

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO 'ABIRI' na 'ABIRIA'

Neno abiri katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:

1. *Nomino* : Harufu nzuri inayonukia; manukato ya kupendeza.

2. *Kitenzi elekezi:*
(i) fafanua jambo kwa vizuri, (ii) eleza jambo litakavyojiri; tabiri.

3. *Kitenzi si elekezi:*
(i) safiri kutoka eneo moja kwenda jingine kwa kutumia chombo chochote cha usafiri.
(ii) fanya safari kwa chombo cha majini.

4. *Kitenzi si elekezi:* elimika na jambo kwa kutumia mfano uliokwishatokea. (Visawe: tahadhari; jihadhari; kuwa mwangalifu.)

5. *Kitenzi si elekezi:* ingia katika chombo cha kusafiri, kwa mfano, meli, basi, mashua na kadhalika.

Neno *abiria* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino* yenye maana ya: mtu anayetoka mahali fulani na kwenda pengine kwa kutumia chombo kwa mfano, basi, treni na kadhalika na ambaye si mfanyakazi wa chombo hicho.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *abiri* limetokana na vitenzi vya Kiarabu *abara* *عبر*  na pia *abbara* *عبر* vyenye maana zifuatazo:

1. Amevuka (barabara au mto).

2. Amesafiri na chombo cha majini.

3. Amekufa/Amefariki/Ametawafu.

4. Amepita/Yamepita.

5. Ameieleza vyema habari fulani.

6. Amefasiri ndoto. 

Kinachodhihiri ni kuwa neno hili ( *abara* *عبر*) lilipoingia katika lugha ya Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *abiri* , maana yake katika lugha ya asili - Kiarabu haikubadilika ingawa lilichukua baadhi za maana na kuacha maana zingine.

Ama neno *abiria* , hili si neno halisi la Kiarabu bali ni matokeo ya usanifishaji na unyambulishaji wa neno *abiri* kutoka neno la Kiarabu *abara/abbara.*

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*