MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
WAZARAMO WALIITAWALA ZANZIBAR KABLA YA MWARABU - Printable Version
JIFUNZE KISWAHILI
WAZARAMO WALIITAWALA ZANZIBAR KABLA YA MWARABU - Printable Version

+- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz)
+-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1)
+--- Forum: Je, wajua ? (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=71)
+--- Thread: WAZARAMO WALIITAWALA ZANZIBAR KABLA YA MWARABU (/showthread.php?tid=1722)



WAZARAMO WALIITAWALA ZANZIBAR KABLA YA MWARABU - MwlMaeda - 12-12-2021

WAZARAMO WALIITAWALA ZANZIBAR KABLA YA MWARABU

Na Maalim Kondo Bungo

Historia zinazofutwa kwa kuficha ukweli ndiyo hizi, kumezuka gumzo mitaani kwa ndugu Hasa A Kingo Mzaramo wa Msanga kuteuliwa kuwa Jaji kule nchini Marekani
Si jambo la kushangaza sana kwani kabila la wazaramo wana mengi waliyowahi kuyafanya makubwa na yenye historia kubwa hapa ulimwenguni
Zanzibar kabla ya kupinduliwa na Waarabu mwishoni mwa karne ya 17 au mwanzoni mwa karne ya 18
Hapo nyuma walitawala watawala weusi akiwemo wa mwisho aliyepinduliwa na Waarabu alikuwa akiitwa Mwinyimkuu ni mzaramo mwenye asili ya Bagamoyo wenyeji wa Zanzibar wanajua eneo la mji mkongwe upo msikiti hasaa unaojulikana wa Mwinyimkuu na pembeni yake kuna Hoteli inayodaiwa ndiyo ilikuwa Ikulu yake.
Ikumbukwe tu Zanzibar uisilamu ulikuja zamani sana kabla Waomani hawajaingia kutawala, uisilamu uliingizwa na Waarabu wa Yemen ambao hawakutaka mambo ya utawa wao ni biashara na Dini tu.
Na walikuja ukanda huo wa Zanzibar na Bagamoyo, kule Bagamoyo wa Yemeni walipewa majina kama Shomvi na Guo kutokana na biashara zao za kuuza chumvi na Nguo wakitembeza mitaani huku wakinadi (Shonvi Shonvi) wakimaanisha Chumvi Chumvi hata kizazi chao walichozaa na waafrika kiliendelea kuitwa Wamashomvi na ukisikia Mzaramo anaitwa Shonvi imetokea huko.
Kwa Zanzibar ilikuwa maamkizi ya wazee wetu mbele ya Mwinyimkuu ni kumwambia: Mwinyi yeye anaitikia Muungwana baada ya kupinduliwa na Waarabu kutoka Oman mwinyi alikuwa mnyonge sana kiasi wafuasi wake walikuwa wakimtembelea wakimwambia: mwinyi yeye akawa anaitikia: mwinyimkuu Said akimkusudia Said Barghash aliyempindua.
Salamu hii inaendelea mpaka leo baadhi ya miji ya pwani hususan uzaramoni Bagamoyo na Kisarawe.
Neno shikamoo na marhaba yalililetwa na mzungu gavana wa Tanganyika na Said Said mtawala wa Zanzibar.
Siku walipokutana Gavana alimpa mkono Sultani Said Said Sultani alipoushika mkono wa Gavana akawa anautikisa Gavana akawa anasema (shake more) akimaanisha tikisa zaidi Sultani akawa anamjibu akitamka (marhabba) kwa maana ya karibu au makaribisho mema wale watu weusi wapambe wa Sultan Said Said wakainasa hiyo ikawa na wao wakija asubuhi wanampa mkono huku wakitamka shake more Sultan anawaitikia vile vile marhabba marhabba, shake more kwa matamshi ya wazee wetu ndiyo ikawa shikamoo na Marahaba ikawa kila unapokutana na mkubwa au kiongozi unamtamkia Shikamoo naye anakuitikia marahaba.

Niwatakie siku Njema